هِمْ بِالحَبِيبِ مُحَمَّدٍ وَذَوِيهِ
إِنَّ الهُيَامَ بِحُبِّهِ يُرْضِيهِ
Mpende Mpenzi Muhammad ﷺ na Familia Yake Tukufu
Kupenda kwake kunamridhisha
إِنْ مَاتَ جِسْمُكَ فَالْهَوَىٰ يُحْيِيهِ
جَسَدٌ تَمَكَّنَ حُبُّ أَحْمَدَ فِيهِ
Hata kama mwili wako utakufa, upendo unaufufua
Mwili ambao upendo wa Ahmad ﷺ umejikita
تَاللّٰهِ إِنَّ الأَرْضَ لَا تُبْلِيهِ
Naapa kwa Allah! ardhi haitauharibu
طُوبَىٰ لِمَنْ هُوَ فِي المَحَبَّةِ صَبُّهُ
لِمَ لَا وَمَوْلَاهُ الكَرِيمُ يُحِبُّهُ
Heri kwa yule ambaye moyo wake umejaa upendo
Kwa nini isiwe hivyo, wakati Mola wake Mkarimu anampenda
فِي القَبْرِ حَاشَا أَنْ يُضَامَ مُحِبُّهُ
أَوْ كَيْفَ يَأْكُلُهُ التُّرَابُ وَحُبُّهُ
Kaburini, mpenzi hatadhalilishwa,
Vipi udongo utamla, wakati upendo wake
فِي قَلْبِهِ وَمَدِيحُهُ فِي فِيهِ
Upo moyoni mwake na sifa midomoni mwake
مَنْ بُعدِهِ رُوحِي أَطَالَتْ أَنَّهَا
أَنَالسَتْ أَصْغِي لِلْعَذُولِ وَإِنْ نَهَىٰ
Kutokana na kutengana, roho yangu imechoka,
Sitasikiliza mkosoaji, hata kama atanikataza.
يَاعَاشِقًا ذَاتَ الحَبِيبِ وَحُسْنَهَا
أَكْثِرْ عَلَيْهِ مِنَ الصَّلَاةِ فَإِنَّهَا
Ewe mpenzi wa kiini na uzuri wa Mpenzi,
Ongeza sala zako juu yake, kwa hakika,
هِيَ نُورُ قَبْرِكَ عِنْدَمَا تَأْوِيهِ
ni mwangaza wa kaburi lako unapoingia
يَا رَبِّ عَبْدٌ قَدْ أَسَا بِفِعَالِهِ
وَبِذُلِّهِ قَدْ مَدَّ كَفَّ سُؤَالِهِ
Ewe Mola! Mtumishi ambaye amekosea katika matendo yake,
Na kwa unyenyekevu wake, ameunyoosha mkono wa ombi lake,
وَأَتَىٰ حَبِيبَكَ طَامِعًا بِنَوَالِهِ
عَبْدٌ تَوَسَّلَ بِالنَّبِيِّ وَآلِهِ
Anamkaribia Mpenzi Wako, akitumaini neema yake,
Mtumishi ambaye anatafuta uombezi kupitia kwa Mtume na familia yake
فَبِحَقِّهِمْ يَا رَبِّ لَا تُخْزِيهِ
Kwa haki yao, Ewe Mola, usimdhalilishe.