مَا لِي سِوَاكْ هَمْ وَأَنْتَ تَعْلَمْ
Sina hamu ila wewe nawe unajua.
Sw
مَا لِي سِوَاكْ هَمْ وَأَنْتَ تَعْلَمْ
فَالْقُرْبُ مَغْنَمْ وَالْبُعْدُ مَغْرَمْ
Sina haja isipokuwa Wewe nawe unajua
Kwani ukaribu ni faida na umbali ni hasara
خُذْنِي إِلَيْكَ بَيْنَ يَدَيْكَ
حُسِبْتُ عَلَيْكَ فِي كُلِّ مَا أَعْلَمْ
Nitwae Kwako mbele Yako
Nimehesabiwa Kwako katika kila nijualo
أَنْتَ مُرَادِي فَكُنْ لِيْ هَادِي
فَالْقَلْبُ صَادِي فَزِلْ لِيْ ذَا الْهَمْ
Wewe ndiye lengo langu basi uwe mwongozaji wangu
Kwani moyo una kiu, niondolee huzuni hii
مَنْ ذَا يَكُنْ لِي إِنْ لَمْ تَكُنْ لِي
تَرَى لِذُلِّي وَأَنْتَ أَرْحَمْ
Nani atakuwa nami ikiwa Wewe huko nami
Unaona unyonge wangu na Wewe ni Mwingi wa Rehema
كَمْ ذَا أُنَادِي يَا خَيْرَ هَادِي
يَكْفِي بُعَادِي فَالْجُودُ قَدْ عَمْ
Mara ngapi nalingania, Ewe mbora wa waongozi
Inatosha kutengana, kwani ukarimu umeenea
نُورُ الْوِصَالِ مَهْرُهُ غَالِي
سِوَاكَ مَا لِي جُدْ وَتَكَرَّمْ
Nuru ya muunganiko mahari yake ni ghali
Sina mwingine ila Wewe, nifadhili kwa ukarimu
قُرْبِي وَبُعْدِي سِيَّانِ عِنْدِي
لِأَنَّ رُشْدِي فِيمَا تَقَسِّمْ
Ukaribu na umbali ni mamoja kwangu
Kwani uongofu wangu upo katika ulichonigawia
فَاجْعَلْ هِبَاتِي رُوحَ الْحَيَاةِ
حَبِيبْ ذَاتِي طه الْمُعَلِّمْ
Basi yajalie mapaji yangu yawe roho ya uzima
Mpenzi wa nafsi yangu, Taha mwalimu
تَعْلَمْ لِقَصْدِي حِبِّي وَوُدِّي
فَكُنْ لِلْكُرْدِي فِي كُلِّ مَغْنَمْ
Unajua kusudio langu, pendo na mahaba yangu
Basi uwe na al-Kurdī katika kila ufanisi
صَلَاةُ رَبِّي لِحَبِيبِ قَلْبِي
طه الْمُرَبِّي عَلَيْهِ سَلَّمْ
Rehema za Mola wangu kwa mpenzi wa moyo wangu
Taha mlezi, amani iwe juu yake