عَطْفَةً يَا جِيرَةَ ٱلْعَلَمِ
Huruma, Ee Majirani wa Patakatifu
Sw
Sw
عَطْفَةً يَا جِيرَةَ ٱلْعَلَمِ
يَا أُهَيْلَ ٱلْجُودِ وَٱلْكَرَمِ
Tazama kwa rehema enyi majirani wa alama tukufu
Enyi watu wa ukarimu na fadhila
نَحْنُ جِيرَانٌ بِذَا ٱلْحَرَمِ
حَرَمِ ٱلْإِحْسَانِ وَٱلْحَسَنِ
Sisi ni majirani katika eneo hili takatifu
Eneo takatifu la wema na uzuri
نَحْنُ مِنْ قَوْمٍ بِهِ سَكَنُوا
وَبِهِ مِنْ خَوْفِهِمْ أَمِنُوا
Sisi ni miongoni mwa watu walioishi humo
Na ndani yake wakapata amani dhidi ya khofu zao
وَبِآيَاتِ ٱلْقُرَانِ عُنُوا
فَٱتَّئِدْ فِينَا أَخَا ٱلْوَهَنِ
Na kwa aya za Qur'ani wakajishughulisha
Basi kuwa mpole kwetu, ewe ndugu wa udhaifu
نَعْرِفُ الْبَطْحَا وَتَعْرِفُنَا
وَالصَّفَا وَالْبَيْتُ يَأْلَفُنَا
Twaijua Batha na yenyewe yatujua
Na Safa na Nyumba Tukufu zatufahamu
وَلَنَا الْمُعْلَا وَخَيْفُ مِنَى
فَاعْلَمَنْ هَذَا وَكُنْ وَكُنِ
Pia tuna makaburi ya Mu'alla na Khaif ya Mina
Basi jua hili kwa yakini
وَلَنَا خَيْرُ الْأَنَامِ أَبُ
وَعَلِيُّ الْمُرْتَضَى حَسَبُ
Na baba yetu ni mbora wa viumbe vyote
Na Ali al-Murtadha ndiye fahari ya nasaba yetu
وَإِلَى السِّبْطَيْنِ نَنْتَسِبُ
نَسَبًا مَا فِيهِ مِنْ دَخَنِ
Na kwa wajukuu wawili tunanasibika
Nasaba isiyo na doa lolote
كَمْ إِمَامٍ بَعْدَهُ خَلَفُوا
مِنْهُ سَادَاتٌ بِذَا عُرِفُوا
Ni maimamu wangapi baada yake walifuata
Mabwana waliojulikana kwa sifa hii
وَبِهَذَا الْوَصْفِ قَدْ وُصِفُوا
مِنْ قَدِيمِ الدَّهْرِ وَالزَّمَنِ
Na kwa sifa hii wameelezewa
Tangu zama za kale hadi leo hii
مِثْلِ زَيْنِ الْعَابِدِينَ عَلِي
وَابْنِهِ الْبَاقِرِ خَيْرِ وَلِي
Mfano wa Ali Zayn al-Abidin
Na mwanawe al-Baqir, mpenzi mbora wa Allah
وَالْإِمَامِ الصَّادِقِ الْحَفِلِ
وَعَلِيٍّ ذِي الْعُلَا الْيَقِنِ
Na Imamu al-Sadiq mwenye sifa nyingi sifiwa
Na Ali mwenye daraja ya juu na yakini
فَهُمُ الْقَوْمُ الَّذِينَ هُدُوْا
وَبِفَضْلِ اللهِ قَدْ سَعِدُوا
Basi hao ni watu walioongoka vyema
Na kwa fadhila za Allah wakapata heri
وَلِغَيْرِ اللهِ مَا قَصَدُوا
وَمَعَ الْقُرْآنِ فِي قَرَنِ
Hawakukusudia mwingine asiyekuwa Allah
Na pamoja na Qur'ani wameambatana daima
أَهْلُ بَيْتِ الْمُصْطَفَى الطُّهْرِ
هُمْ أَمَانُ الْأَرْضِ فَادَّكِرِ
Watu wa nyumba ya Mustafa aliye mtukufu
Wao ni amani ya ardhi, basi kumbuka hili
شُبِّهُوا بِالْأَنْجُمِ الزُّهْرِ
مِثْلَ مَا قَدْ جَاءَ فِي السُّنَنِ
Wamefananishwa na nyota zenye kung'ara
Kama vile ilivyokuja katika hadithi za Mtume
وسَفِنٌ لِلنَّجَاةِ إِذَا
خِفْتَ مِنْ طُوفَانِ كُلِّ أَذَى
Nao ni majahazi ya wokovu pindi
Utakapohofia gharika ya kila adha
فَانْجُ فِيهَا لَا تَكُونُ كَذَا
وَاعْتَصِمْ بِاللهِ وَاسْتَعِنِ
Basi okoka kwayo wala usitengane nao
Na mshike Allah na uombe msaada Wake
رَبِّ فَانْفَعْنَا بِبَرْكَتِهِمْ
وَاهْدِنَا الحُسْنَى بِحُرْمَتِهِمْ
Mola wetu tunufaishe kwa baraka zao
Na tuongoe kwenye kheri kwa utukufu wao
وَأَمِتْنَا فِي طَرِيقَتِهِمْ
وَمُعَافَاةٍ مِنَ الفِتَنِ
Na tufishe katika njia yao
Hali ya kusalimika na kila fitina
ثُمَّ لَا تَغْتَرَّ بِالنَّسَبِ
لَا وَلَا تَقْنَعْ بِــكَانَ أَبِي
Kisha usidanganyike na nasaba yako
Wala usitosheke na kusema "Baba yangu alikuwa"
وَاتَّبِعْ فِي الهَدْيِ خَيْرَ نَبِي
أَحْمَدَ الهَادِي إِلَى السُّنَنِ
Bali fuata katika uongofu mbora wa Manabii
Ahmad, kiongozi wa njia ya Mtume
فَهُوَ خَتْمٌ لِلنَّبِيِّينَا
وَإِمَامٌ لِلْمُطِيعِينَا
Kwani yeye ni hatima ya Manabii wote
Na kiongozi wa watu watiifu
وَلِساَنٌ لِلْمُجِيبِينَا
يَوْمَ نُودُوا خَيْرَ مُؤْتَمَنِ
Msemaji kwa niaba ya waja wote watiifu
Na mbora wa kuombwa msaada siku ya malipo
صَلَوَاتُ اللهِ ذِي الكَرَمِ
تَتَغَشَّى المُصْطَفَى العَلَمِ
Rehema za Allah Mwenye ukarimu
Zimfunike Mustafa, alama kuu ya uongofu
مَا سَرَى رَكْبٌ إِلَى الحَرَمِ
وَصَبَا صَبٌّ إِلَى سَكَنِ
Maadamu msafara unaelekea Haramuni
Na mpenzi akitamani makazi yake
وَعَلَى آلِ النَّبِيِّ الكُرَمَا
وَعَلَى أَصْحَابِهِ العُلَمَا
Na pia kwa Aali wa Nabii wakarimu
Na kwa maswahaba zake walio wanachuoni
وَعَلَى أَتْبَاعِهِ الحُكَمَا
وَأُولِي الأَلْبَابِ وَالفِطَنِ
Na kwa wafuasi wake wenye hekima
Na wenye akili na ufahamu wa ndani